首页 Lum 180;at-ul-I 180;tiqaad – Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy

Lum 180;at-ul-I 180;tiqaad – Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy

举报
开通vip

Lum 180;at-ul-I 180;tiqaad – Imaam Ibn Qudaamah al-MaqdisiyLum 180;at-ul-I 180;tiqaad – Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy ?,,??,? ?,,? Lum?at-ul-I?tiqaad [Mwanga wa I?tiqaad] Mwandishi: ??~,,?? ?,?~, ??? ???,?? ?,,,? Imaam Muwaffiq-ud-Diyn Ibn Qudaamah al-Maqdisi...

Lum  180;at-ul-I  180;tiqaad – Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy
Lum 180;at-ul-I 180;tiqaad – Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy ?,,??,? ?,,? Lum?at-ul-I?tiqaad [Mwanga wa I?tiqaad] Mwandishi: ??~,,?? ?,?~, ??? ???,?? ?,,,? Imaam Muwaffiq-ud-Diyn Ibn Qudaamah al-Maqdisiy Tarjama (na maelezo ni): Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush 1 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy Dibaji .......................................................................................................................................................................................... 4 Ibn Qudaamah al-Maqdisiy alikuwa nani? ........................................................................................................................ 7 Utangulizi................................................................................................................................................................................. 10 Kuamini Majina na Sifa za Allaah ..................................................................................................................................... 10 Elimu ya wajibu kuhusiana na Majina na Sifa za Allaah ............................................................................................. 11 Aayah za Mutashaabih ......................................................................................................................................................... 11 Maimamu wa Salaf kuhusu Sifa za Allaah ...................................................................................................................... 13 Maamrisho ya kushikamana na Sunnah, hadhari ya Bid?ah na kauli za maulamaa kuhusiana na hilo ........... 16 Mfano wa Sifa za Allaah zilizothibitishwa na Qur-aan na Sunnah .......................................................................... 18 Dalili ya uso wa Allaah .................................................................................................................................................... 19 Dalili ya mikono ya Allaah ............................................................................................................................................. 19 Dalili ya nafsi ya Allaah................................................................................................................................................... 19 Dalili ya kuja kwa Allaah ................................................................................................................................................ 19 Dalili ya kuridhia na kupenda kwa Allaah.................................................................................................................. 20 Dalili ya kukasirika na kughadhibika kwa Allaah ..................................................................................................... 20 Dalili ya kustaajabu kwa Allaah .................................................................................................................................... 21 Dalili ya kucheka kwa Allaah......................................................................................................................................... 21 Dalili ya kwamba Allaah yuko juu ya mbingu na viumbe...................................................................................... 22 Dalili ya maneno ya Allaah na uwajibu wa kuthibitisha hilo...................................................................................... 24 Qur-aan ni maneno ya Allaah hakika ............................................................................................................................... 26 Waumini watamuona Mola Wao siku ya Qiyaamah .................................................................................................... 29 Qadhwaa? na Qadar.............................................................................................................................................................. 30 Imani ni maneno na ?amali na inazidi na kupungua .................................................................................................... 32 Kuamini ghaibu na yote yaliyosema Mtume .................................................................................................................. 33 Pepo, Moto na kifo ni haki ................................................................................................................................................. 35 Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) ndio wa mwisho na haki zake na Maswahabah wake................... 35 Kupigana Jihaad na viongozi wote, sawa wakiwa ni wema au waovu .................................................................... 38 2 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy Imani ya Salaf kwa Maswahabah na yule mwenye kuwaponda ................................................................................ 38 Imani ya Salaf kwa wakeze Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) .................................................................. 39 Haki za watawala kwa raia................................................................................................................................................... 39 Msimamo wa Ahl-us-Sunnah kwa Ahl-ul-Bid?ah......................................................................................................... 40 Tofauti katika matawi ........................................................................................................................................................... 41 Hitimisho ................................................................................................................................................................................. 42 3 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy Dibaji Himdi zote anastahiki Allaah. Swalah na salaam zimwendee Mtume wetu Muhammad, kizazi chake na Maswahabah zake, amma ba?d: Shaykh Swaalih Aalush-Shaykh (Hafidhwahu Allaah) amesema: "Hichi ni kitabu kinachoitwa "Lum?at-ul-I?tiqaad" ni katika vitabu vifupi kuhusu ?Aqiydah. Kimezungunzia masuala ya ?Aqiydah na wanachuoni baada ya mtunzi wa kitabu wamekisifu sana. Mambo ya ?Aqiydah kwa Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa?ah yamejengwa juu ya kufafanua misingi sita ya Iymaan, nayo ni kumuamini Allaah, Malaika Wake, Vitabu Vyake, Mitume Wake, siku ya Mwisho na Qadar - kheri na shari yake - ni yenye kutoka kwa Allaah (Ta?ala). Kumuamini Allaah kumejumuisha ndani yake kuamini kuwa Allaah ni Mmoja katika uungu Wake na Yeye ndiye mwenye kustahiki kuabudiwa pasi na mwengine, kuamini majina na sifa Zake (Jalla wa ?Alaa) na kwamba Yeye amepwekeka katika hayo, hakuna anayeshabihiana na kufanana Naye. Mwanzoni mwa Uislamu, katika zile karne za kwanza, hakukuwepo haja ya kuitenga Tawhiyd-ul-Uluuhiyyah kivyake kwa njia ya upambanuzi pindi kulipokuwa kunazungumziwa mada hii, yaani kumuamini Allaah. Badala yake mtu alikuwa anatosheka kufafanua imani hii kwa jumla ili waislamu wasije wakatumbukia katika shirki na ilili shirki isije kudhihiri. Kwa hivyo vitabu vingi vya ?Aqiydah vyenye kuzungumzia juu ya kumuamini Allaah karibu vyote vilikuwa vinahusu majina na sifa za Allaah. Kwa ajili hiyo ndio maana hutopata katika kitabu hichi kumezungumziwa kwa upambanuzi juu ya Tawhiyd-ul-Uluuhiyyah. Hili walilifanyia kazi wanachuoni waliokuja baada ya kufa kwa mtunzi wa kitabu. Hata hivyo utapata kumezungumziwa kwa upambanuzi juu ya majina na sifa za Allaah. Hili ni kutokana na haja ya hilo katika zama za mtunzi wa kitabu hichi. Kadri na jinsi waja wana haja ya kufafanuliwa zaidi jambo fulani, ndivyo jinsi wanachuoni walivyolitendea kazi kwa bidii. Kwa ajili hiyo wakaandika vitabu kuhusu Tawhiyd-ul-Uluuhiyyah, kwa mfano Kitaab-ut-Tawhiyd, Kash-ush-Shubuhaat, Thalaathat-ul-Usuwl na mfano wake. Kwa sababu ya kukidhi haja ya kipindi hicho vitabu hivi vikafafanua Tawhiyd-ul- 4 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy Uluuhiyyah, msingi wa nguzo ya kwanza ya kuamini, ambayo ni kumuamini Allaah. Baada ya hapo mwandishi akataja kuwaamini Malaika, Vitabu Vyake, Mitume Wake, siku ya Mwisho na Qadar kheri na shari yake. Baada ya kufafanuliwa nguzo sita za imani, mwandishi akataja mambo zaidi kuhusu I?tiqaad. Mambo hayo hayana lolote kuhusiana na I?tiqaad, lakini yameingizwa katika mambo ya ?Aqiydah kwa sababu Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa?ah wameenda kinyume na Ahl-ul-Bid?ah wal-Furqah katika mambo hayo. Mfano wa mambo hayo ni kama kuwazungumzia Maswahabah, mama wa Waumini na haki zao. Mwandishi ametaja pia kuhusu uongozi katika Uislamu na yale mambo yenye kuwawajibikia watawala na wananchi; mambo ambayo Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa?ah wametofautiana kwayo na Khawaarij, Mu?tazilah na watu mfano wao. Vilevile Ahl-us-Sunnah wameingiza kupangusa juu ya soksi katika mambo ya ?Aqiydah. Hili ni kwa sababu ya kwenda kinyume na wale wenye kuonelea kuwa kupangusa juu ya soksi si sahihi. Kadhalika wametaja karama za mawalii na yale Allaah anayoyapitisha kupitia mikono yao katika mambo mbalimbali ya elimu, ya ajabu, ya uwezo na yenye kuathiri. Haya yametajwa kwa upambanuzi na kufafanuliwa kwa sababu kuna ambao wanaenda kinyume na karama hizi, ima kwa kuzikanusha, kama wanavyofanya Mu?tazilah, au kupetuka mipaka kwa mawalii kiasi cha kwamba kuna waliowafanya nafasi za mawalii zikawa juu ya za Mitume. Kadhalika mambo ya maadili yanatajwa katika mambo ya ?Aqiydah ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa?ah. Kwa hivyo ?Aqiydah ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa?ah imekusanya mambo yote haya na haihusiani peke yake na kuamini majina na sifa za Allaah, siku ya Mwisho na Qadar kheri na shari yake. Bali ?Aqiydah ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa?ah imekusanya mambo yote haya, kwa sababu wao katika mambo haya wametofautiana na Ahl-ul-Bid?ah waz-Zaygh ambao wanayarudisha Maandiko, na wala hawafuati Sunnah na hawaachi wakahukumiwa kwavyo kuhukumiwa kikamilifu. Kwa njia hiyo Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa?ah wakawa ni wenye sifa za kipekee kwa sababu 5 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy wanaiadhimisha Sunnah na watu wake na wanawakosoa wale wenye 1kwenda nayo na kwenda kinyume na maimamu wao..." 1 Kutoka katika mkanda "Sharh Lum?at-il-I?tiqaad" (01), Tasjiylaat Ibn Taymiyyah Khubar, Saudi Arabia 6 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy Ibn Qudaamah al-Maqdisiy alikuwa nani? Jina: Alikuwa ni Imaam, Faqiyh, Zaahid na Shaykh-ul-Islaam Muwaffiq-ud-Diyn Abu Muhammad ?Abdullaah bin Ahmad bin Muhammad bin Qudaamah bin Miqdaam bin Naswr bin ?Abdillaah al-Maqdisiy, halafu ad-Dimashqiy, as-Swaalih. Kazaliwa katika mwezi wa Sha?abaan mwaka wa 541 baada ya Hijrah katika kijiji Jammaa?iyl kwenye jimbo la Nablus karibu na Jerusalemu. Kukua kwake: Alienda pamoja na familia yake Dameski wakati alikuwa na miaka kumi. Huko ndio alisoma na kuhifadhi Qur-aan na mukhtaswar wa andiko la “al- Khiraqiy”. Alipokuwa na miaka ishirini alisafiri kwenda Baghdaad pamoja na familia na binamu yake Imaam ?Abdul-Ghaniy al-Maqdisiy (Rahimahu Allaah) na akakaa na kusikiliza wanachuoni wa hapo mjini. Uchaji Allaah wake na kujiepusha kwake na mambo ya anasa: Alikuwa ni mchaji Allaah, mwenye kujiepusha na anasa na mwenye hadhi na subira na mwenye kutumia siku zake katika kusoma na kufanya ?amali. Pindi anapojadili, alikuwa akijadili kwa hoja na dalili. Alikuwa hawadharau watu na wala kukasirika. Waalimu wake: Imaam Ibn Qudaamah (Rahimahu Allaah) alisoma kwa idadi kubwa ya waalimu. Maarufu alikuwa ni Taqiyy-ud-Diyn Abu Muhammad ?Abdul-Ghaniy al-Maqdisiy na Faqiyh mwanachuoni mkubwa wa ?Iraaq, Naasih-ul- Islaam Abul-Fath Naswr bin Fatyaan, na maarufu zaidi kama Ibn-ul-Munaa. Baghdaad alisoma Imaam Ibn Qudaamah kwa Shaykh ?Abdul-Qaadir al-Jiylaaniy. Wanafunzi wake: 7 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy Alikuwa na wanafunzi wengi sana. Waliokuwa maarufu ni Shihaab-ud-Diyn Abu Shaamah al-Maqdisiy na Zakiyy-ud-Diyn Abu Muhammad al-Mundhiriy. Maimamu kuhusu Imaam Ibn Qudaamah: Imaam Ibn-us-Salaah kasema: “Sijawahi kuona mtu kama Shaykh Muwaffiq-ud-Diyn.” Imaam Ibn Taymiyyah kasema: “Baada ya al-Awzaa?iy hakuna Faqiyh mwengine kuliko Shaykh Muwaffiq-ud-Diyn alivyoingia Shaam.” Imaam al-Mundhiriy kasema: “Alikuwa Faqiyh, Imaam... " Imaam adh-Dhahabiy kasema: “Alikuwa mmoja katika maimamu wa ajabu sana na mwandishi wa vitabu." Imaam Ibn Kathiyr kasema: “Alikuwa Shaykh-ul-Islaam, Imaam, mjuzi na bingwa. Hakuna aliyekuwa mjuzi kuliko yeye katika Fiqh, wakati wa zama zake au kipindi kirefu kabla yake.” Vitabu vyake: Katika Fiqh: al-Mughniy, al-Kaafiy, al-?Umdah, al-Muqni? na vyengine. Katika ?Aqiydah: Lum?at-ul-I?tiqaad (Mwanga wa I?tiqaad), al-Qadr, Dham-ut-Ta?wiyl na vyengine. Katika Usuul-ul-Fiqh: Rawdhwat-un-Naadhir na vyengine. Katika Raqaa?iq na Zuhd: ar-Riqqah wal-Bukaa? na at-Tawwaabuun. 8 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy Katika Hadiyth: Mukhtaswar ?Ilal-il-Khallaal na vyengine. Elimu na khabari zaidi kuhusu Shaykh-ul-Islaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy (Rahimahu Allaah), tazama: “Taariykh-ul-Islaam (669) na “Siyar A?alaam-in-Nubalaa" ya (22/165-173) Imaam adh-Dhahabiy (Rahimahu Allaah). “al-Bidaayah wan-Nihaayah (13/99-100) ya Imaam Ibn Kathiyr (Rahimahu Allaah). “Dhayl Twabaqaat-il-Hanaabilah" (2/122-149) ya Imaam Ibn Rajab (Rahimahu Allaah) “Fihris Makhtwuutwaat-idh-Dhwaahiriyyah" ya Imaam al-Albaaniy (Rahimahu Allaah) 9 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy Utangulizi Himdi zote zinamstahikia Allaah Mwenye kusifiwa na kila ulimi na Mwenye kuabudiwa katika kila zama. Ambaye elimu Yake imeenea kila mahali na wala Hashughulishwi na kitendo kutokana na kitendo kingine. Ametakasika kuwa na vyenye kumshabihi, washirika, wake na watoto. Hukumu Yake inawazunguka waja wote. Akili/mawazo hayawezi kumtambua kwa kumfikiria na wala nyoyo haziwezi kumdhibiti kwa kumuelezea: ????,????? ?,??,,??? ???,?? ? ?????, ?,???,?,?, ?????? ”Hakuna chochote kinachofanana Naye - Naye ni Mwenye kusikia, Mwenye kuona.” (42:11) Kuamini Majina na Sifa za Allaah Ana majina mazuri na sifa kuu: ?,,,???, ?????,????? ?????,?? ,?? ????,,?? ???,?? ????? ??,???,???? ????? ?,?:?,??? ??, ????? ???????,,??? ??, ??? ?,?? ????????? ?????,??? ????, ?,???,?,,??? ??,?,???? ,?????? ?????,?? ”Mwingi wa Rahmah amelingana juu ya ?Arshi. Ni Vyake Pekee vyote vilivyomo mbinguni na vilivyomo ardhini na vilivyomo baina yake na vile vilivyomo chini ya udongo. Na ukinena kwa jahara; basi [tambua kuwa] Yeye anajua ya siri na yanayofichika zaidi.” (20: 5-7) Elimu Yake imekizunguka kila kitu. Vilevile ana ufalme juu ya viumbe wote kwa hukumu, huruma na elimu Yake imekienea kila kitu: ??,???, ?,?? ?,??,??,?? ????? ?????,???, ????? ??????~???? ?,???? ??? ?????,?? "Anajua yale yaliyoko mbele yao, na yale yaliyoko nyuma yao na wala 10 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy hawawezi kumzunguka kwa kumtambua.” (20:110) Elimu ya wajibu kuhusiana na Majina na Sifa za Allaah Anasifiwa kwa yale Aliyojisifia Mwenyewe katika Kitabu Chake Kitukufu na kupitia Mtume Wake (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) mtukufu. Kila kilichokuja katika Qur-aan au kimesihi kutoka kwa Mteuliwa (?alayhis-Salaam) kuhusiana na sifa za Mwingi wa Rahmah, basi ni wajibu kukiamini na kukipokea kwa kujisalimisha na kukikubali, na kuacha kuyatupilia mbali, kuyafasiri kimakosa, kuyashabihisha na kuyafananisha. Aayah za Mutashaabih 2Kuhusiana na yanayotatiza katika hayo, ni wajibu kuyathibitisha 3 na kuacha kuyaingilia sana ndani maana. Sambamba na hilo kimatamshi 2 Shaykh Muhammad bin Swaalih bin ?Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) amefafanua kuhusu kutatiza kwa maandiko na kusema ifuatayo: "Hakika suala la dalili za Qur-aan na Sunnah kuwa wazi na kutatiza linakuja kwa baadhi ya watu pasi na wengine. Watu wanatafautiana kutegemea na elimu na ufahamu. Andiko fulani linaweza kuwa lenye kutatiza kwa mmoja na wakati huo huo kwa mwengine likawa liko wazi. Katika hali kama hii la wajibu pindi andiko linapotatiza ni kama tulivyotangulia kusema mtu asiliingilie na kupekua maana yake. Kuhusu uhakika wa Maandiko ya Kishari?ah yenyewe kama Maandiko ndani yake hakuna kitu chenye kutatiza ambacho hakuna yeyote asiyejua maana yake katika yale mambo yenye kuwahusu miongoni mwa mambo ya dini na dunia yao. Hilo ni kwa sababu Allaah ameisifu Qur-aan kuwa ni nuru ya wazi, ubainifu kwa watu na ni pambanuo. Vilevile ameisifu kuwa ameiteremsha ikiwa ni yenye kukibainisha kila kitu na kwamba ni uongofu na huruma. Haya yanapelekea katika Maandiko kusiweko kitu chenye kutatiza kwa kutegemea na uhalisia kwa njia ya kwamba kusiwepo hata mmoja katika Ummah ambaye hajui maana yake." (Sharh Lum?at-il-I?tiqaad, uk. 33, Adhwaa?-us-Salaf)) 3 Shaykh al-Imaam Muhammad bin Ibraahiym Aal ash-Shaykh (Rahimahu Allaah) amesema kuhusiana na kauli ya mwandishi ”ni wajibu kuyathibitisha lafdhi (matamshi)”: “Hili ambalo limesemwa na mwandishi, ni katika mambo ambayo kakosolewa katika kitabu hichi, kwa kuwa ni maarufu ya kwamba madhehebu ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa?ah ni kuamini yaliyothibiti katika Kitabu na Sunnah kuhusiana na Majina na Sifa za Allaah kwa lafdhi (matamshi) na maana (yaani mtu aamini ya kwamba kilichoandikwa maana yake ni ya uhakika, kwa mfano Mkono maana yake ya uhakika ni Mkono n.k). Kwa imani iliyo imara ijulikane ya 11 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy tunamrudishia ujuzi wake kwa Aliyeyatamka na kujaalia jukumu lake kwa yule aliyelisimulia - hilo ni kwa kufuata njia ya wale wenye msingi madhubuti katika elimu ambao Allaah kawasifu katika Kitabu Chake cha wazi pale aliposema (Subhaanahu wa Ta?ala): ??,????: ?~,?, ?,??? ,??, ?,?? ?,,??? ?,?????,?? ?????,??? ??, ?,??,???,????? “Na wale wenye msingi madhubuti katika elimu husema: “Tumeziamini, zote ni kutoka kwa Mola wetu."" (03:7) Upande mwingine Amewaraddi wale wanaotaka kupotosha na kuharibu Uteremsho Wake wa Aayah zisizokuwa wazi: ?,?,??? ?,??? ?,??????,?? ?????,?? ????? ? ?,??????,?? ????,??????? ???,???,??? ????,????? ?,?,?? ?,????,?? ??? ?,??,??,????, ?,???? ??????????, ??, ?,??,,?? ?,??,?, ”Basi wale ambao katika nyoyo zao mna upotevu hufuata zile zisizokuwa wazi ili kutafuta fitnah na kutafuta kuzipotosha - na hakuna ajuae uhakika Wake isipokuwa Allaah.” (03:7) Amefanya kutafuta kuzipotosha ni alama ya upotevu na Akaliambatanisha hilo na kukusudia kutafuta fitina. Halafu vilevile Akawafungia kwa yale waliyoyatarajia na Akaponda ndoto zao kwa yale waliyoyakusudia pale aliposema (Subhaanah): ?,?,??? ?,??? ?,??????,?? ?????,?? ????? ”Na hakuna ajuae uhakika Wake isipokuwa Allaah.” (03:7) kwamba Majina na Sifa hizi ni za uhakika na za ukweli na sio Majaaz na kwamba hizo zote zina maana ya hakika na kweli inayolingana na Utukufu na Ukubwa wa Allaah... Ama kuhusiana na kayfiyyah namna ya Sifa zilivyo kwa uhakika, ni Allaah (Subhaanah) peke Yake Ndie Azijuae, kwa kuwa kauli ya Sifa maana yake ni kauli kwa yule Mwenye Kuelezwa. Hali kadhalika hakuna yeyote isipokuwa Yeye Mwenyewe ndiye Ajuae Alivyo, hali kadhalika na Sifa Zake – na hii ndio maana ya kauli ya Imaam Maalik “Namna gani haijulikani.”.” (Fataawa wa Rasaa?il Samaahat-ish-Shaykh Muhammad bin Ibraahiym”, (1/202-203)) 12 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy 4Maimamu wa Salaf kuhusu Sifa za Allaah Imaam Abu Abdillaah Ahmad bin Muhammad bin Hanbal (Radhiya Allaahu ?anh) amesema kuhusu maneno ya Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam): 5“Hakika Allaah hushuka katika mbingu ya dunia.”, “Hakika Allaah 67ataonekana siku ya Qiyaamah.” na Hadiyth zinazofanana na hizi: 8“Tunaziamini na kuzisadikisha. Bila ya kuzifanyia namna wala maana na wala haturudishi kitu katika hayo. Kadhalika tunajua kuwa yale yaliyokuja 4 Shaykh ?Abdur-Rahmaan bin Jibriyn (Rahimahu Allaah) amesema: “Salaf (waliotangulia) ni karne bora katika Maswahabah, kisha waliofuata na kisha waliofuata.” (at-Ta?liyqaat ?alaa Matn Lum?at-il-I?tiqaad, uk. 50, Daar-us-Samiy?iy). 5 al-Bukhaariy (1145), (6321) na (7494) na Muslim (758) 6 Muslim (181). 7 Shaykh Muhammad bin Swaalih bin ?Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) kafafanua neno ”Hadiyth” namna ifuatayo: ”Ni maneno, matendo, aliyoyakubali na sifa vilivyonasibishwa kwa Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam).” (Mustwalah-ul-Hadiyth, uk. 07, Maktabah al-Ma?aariyf, Riyaadh). 8 Shaykh Swaalih Aalush-Shaykh (Hafidhwahu Allaah) amesema: "Maneno haya kutoka kwake (Rahimahu Allaah) yamewatatiza baadhi ya watu na kuuliza ni vipi atasema bila ya kuzifanyia namna wala maana. Wamesema kuwa uhakika wa mambo ni kwamba matamshi haya yanaafikiana na madhehebu ya Mufawwidhwah ambao walikuwa wakisema kuwa wanaamini matamshi bila ya maana. Kwa msemo mwingine kwamba Allaah peke yake ndiye anajua maana na namna ya sifa za Allaah. Hii ni I?tiqaad batili na Bid?ah mbaya. Lililo la wajibu ni kumuachia Allaah namna. Kuhusiana na maana iko wazi. Qur-aan imeteremshwa kwa lugha ya kiarabu ilio wazi. Ikiwa Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa?ah wanaamini matamshi ya maana kutokana na vile ambavyo matamshi ya kiarabu yanavyofahamisha, ni vipi basi yatafasiriwa maneno ya Imaam Ahmad: "Bila ya kuzifanyia namna wala maana?" Hili pia ni katika mambo ambayo mwandishi - yaani Ibn Qudaamah - amekosolewa kwa vile hakuweka wazi makusudio ya maneno ya Imaam Ahmad. Wanachuoni wanasema makusudio ya Imaam Ahmad kusema hivo ni kutaka kuraddi mapote mawili: Pote la kwanza: Mushabbihah Mujassimah. Amewaraddi pale aliposema: "... bila ya kuzifanyia namna." 13 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy na Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) ni haki na wala hatumrudi Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam). Hatumsifu Allaah zaidi ya alivyojisifu Mwenyewe – hili tunalifanya bila ya kumuwekea mpaka wala kiwango. ????,????? ?,??,,??? ???,?? ? ?????, ?,???,?,?, ?????? ”Hakuna chochote kinachofanana Naye - Naye ni Mwenye kusikia, Mwenye kuona.” (42:11) Bi maana namna ambayo inafikiriwa na akili za Jahmiyyah au Mumaththilah na wakamsifu Allaah (?Azza wa Jall) kwayo. Pole la pili: Mu?attwilah. Amewaraddi pale aliposema: "... wala maana." Hawa ni wale ambao wamefasiri maana ya maneno ya Qur-aan na Sunnah kinyume na udhahiri wake. Kwa mfano wamesema Allaah kushuka maana yake "rehema za Allaah hushuka", Allaah amelingana maana yake "Allaah ametawala", huruma maana yake ni "kutaka wema" na "kutaka kheri" na ghadhabu za Allaah maana yake ni "kutaka kupatiliza". Wanafasri namna hii. Imaam Ahmad anaposema: "... bila ya kuzifanyia namna..." anachokusudia ni namna waliyomfanyia Mujassimah Allaah (Ta?ala). "... wala maana." bi maana maana inayokusudiwa na Mu?attwilah. Kwa msemo mwingine maana ya batili iliyokusudiwa na wazushi Mu?awwilah. Hapa tunajifunza kanuni ambayo ni muhimu, nayo ni kwamba mwanafunzi ambaye anatilia umuhimu jambo la ?Aqiydah ni lazima aielewe I?tiqaad ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa?ah kikamilifu. Baada ya kuielewa na akakutana na matamshi yenye kutatiza kutoka kwa maimamu wa Taabi?uun na waliokuja baada ya Taabi?uun kutokana na kufahamu kwake ?Aqiydah sahihi anaweza akayafasiri kwenda katika maana iliyonyooka. Kwa sababu isifahamike kuwa Imaam Ahmad - ambaye ndiye imamu wa Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa?ah ambaye aliwahukumu Mufawwidhwah kuwa ni wazushi aliposema: "... wala maana" eti anakusudia kuwa Aayah na Hadiyth hazina maana kabisa. Kwa wewe kufahamu kwako msingi wa I?tiqaad na msingi wanaofuata Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa?ah na kuzama katika hilo utaweza kujibu utatizi mwingi." (Sharh Lum?at-il-I?tiqaad, uk. 38-39, Adhwaa?-us-Salaf)) 14 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy Tunasema kama Alivyosema na tunamsifu kama Alivyojisifia Mwenyewe - hatuvuki hayo. Watu hawawezi kufikia kumjulisha kwa msaada wa maelezo. Tunaamini Qur-aan yote, sawa Aayah zilizo wazi na zisizokuwa wazi. Hatumuondoshei kitu katika sifa Zake, sawa bila ya kujali shutuma za wenye kutushutumu kwa hilo. Hatuvuki Qur-aan na Hadiyth na wala 9hatutambui namna gani zimekuwa hivyo isipokuwa kwa kumsadikisha 10Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) na kuthibitisha Qur-aan. Imaam Abu ?Abdillaah Muhammad bin Idriys ash-Shaafi'iy (Radhiya Allaahu ?anh) amesema: “Nimemuamini Allaah na yaliyokuja kutoka kwa Allaah kama alivyokusudia Allaah. Vilevile nimemuamini Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) na yaliyokuja kutoka kwa Mtume wa Allaah 1112kama alivyokusudia Mtume wa Allaah." 9 Shaykh Ibn Jibriyn (Rahimahu Allaah) amesema: ”Hatujui namna gani Sifa zilivyo, lakini tunazikubali kama ishara ya kwamba tunamuamini Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam), kwa kuwa ni yeye ndie kazisimulia.” (at-Ta?liyq ?alaa Matn Lum?at-il-I?tiqaad, uk. 48, Daar-us-Sami?iy) 10 Tazama Imaam Ibn-ul-Jawziy ”Manaaqib al-Imaam Ahmad”, uk. 156, Imaam adh- Dhahabiy ”Taariykh-ul-Islaam”, uk. 27, Imaam Ibn Muusuliy ”Mukhtaswar as-Sawaa?iq al-Mursalah” (2(251) na Imaam Abu Ya?la ?Ibtaal at-Ta?wiylaat li Akhbaar-is-Swifaat (1/44-45). 11 Tazama Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah ”al-Fataawaa al-Hamawiyyah al-Kubraa”, uk. 121. 12 Shaykh Swaalih Aalush-Shaykh (Hafidhwahu Allaah) amesema: "Tunasema kama alivyosema kwamba, tunamuamini Allaah na yale yaliyokuja kutoka kwa Allaah, sawa yale tuliyoyajua na yale ambayo hatukuyajua, kama alivyokusudia Allaah. Huku ni kujisalimisha kikamilifu na kunyenyekea kikamilifu yale tuliyoamrishwa. Kadhalika tunamuamini Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam), na yale yaliyokuja kutoka kwa Mtume wa Allaah, kama alivyokusudia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam), sawa yale maandiko tuliyoyajua na yale ambayo hatukuyajua. Hii ni imani ya kijuma. Maana yake ni kwamba hatuachi kitu katika yale yenye kutoka kwa Allaah na kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) isipokuwa sisi ni wenye kukiamini. Ni mamoja yale tuliyoyajua na yale ambayo hatukuyajua - yote ni yenye kutoka kwa Mola Wetu. ash-Shaafi?iy amesema maneno haya kwa kujisalimisha na yale Allaah (?Azza wa Jall) aliyoamrisha katika Kitabu Chake aliposema: ??,????: ?~,?, ?,??? ,??, ?,?? ?,,??? ?,?????,?? ?????,??? ??, ?,??,???,?????"Na wale wenye msingi madhubuti katika elimu husema: “Tumeziamini, zote ni kutoka kwa Mola wetu."" (03:07) 15 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy Hii ndio njia waliyopita Salaf na maimamu wa Khalaf (Radhiya Allaahu ?anhum). Wote wamekubaliana kupitisha na kuthibitisha sifa zote zilizothibiti katika Kitabu cha Allaah na Sunnah za Mtume Wake (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) pasi na kuziingilia kwa kuzifasiri kimakosa. Maamrisho ya kushikamana na Sunnah, hadhari ya Bid?ah na kauli za maulamaa kuhusiana na hilo Hakika tumeamrishwa kufuata Aathaar zao na kuwachukua kama kiigizo 13bora kwa kuwaiga. Jengine ni kuwa tumetahadharishwa na Muhdathah na tukaelezwa kwamba ni katika upotevu. Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) amesema: “Jilazimieni na Sunnah zangu na Sunnah za makhaliyfah wangu waongofu baada yangu. Ziumeni kwa magego yenu. Tahadharini na 14mambo ya kuzua! Hakika kila Muhdathah ni Bid?ah na kila Bid?ah ni 15upotevu.” ?Abdullaah bin Mas?uud (Radhiya Allaahu ?anh) amesema: Yale tuliyojua maana yake ni jambo la wazi kuyaamini. Kuhusu yale tusiyoyajua maana yake na yakatutatiza, tunasema kuwa tunayaamini vile alivyokusudia Mola Wetu (?Azza wa Jall) na Mtume wetu (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam). Tunachotakiwa ni kuwauliza wanachuoni. Baada ya kuwauliza wanachuoni na wakatubainishia maana ya Qur-aan na Sunnah hapo ndipo inatakiwa kwetu kuamini maana kama tunavyoamini maandiko." (Sharh Lum?at-il-I?tiqaad, uk. 42-43) 13 Shaykh Ibn Jibriyn (Rahimahu Allaah) amesema kuhusu neno "Muhdathah": "Ni kila ambacho watu wamezua katika dini kilichojengwa juu ya matamanio na maoni na kisichokuwa na msingi katika dini." (at-Ta?liyqaat ?alaa matn Lum?at-il-?I?tiqaad, uk. 53, Daar-us-Samiy?iy) 14 Shaykh Ibn ?Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) amesema kuhusu "Bid?ah": "Bid?ah maana yake kilugha ni kitu chenye kuzuliwa. Bid?ah maana yake kiistilahi ni kile chenye kuzuliwa katika dini ambacho kinapingana na yale aliyokuwa akifuata Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) na Maswahabah zake sawa katika mambo ya ?Aqiydah au matendo." (Sharh Lum?at-il-I?tiqaad, uk. 40, Adhwaa?-us-Salaf) 15 Abu Daawuud (4607), at-Tirmidiy (2678), Ahmad (4/126-127), ad-Daarimiy (1/44-45), Ibn Maajah (42-43), al-Haakim (1/95) na wengine. Imaam Ibn Hibbaan, Imaam al-Ajjurriy na Imaam al-Albaaniy (Rahimahumu Allaah) wamesema kuwa ni Swahiyh. Tazama “Swahiyh al-Jaami? as-Swaghiyr” (2/344) ya Imaam al-Albaaniy (Rahimahu Allaah). 16 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy 1617“Fuata na wala usizue, kwani hakika umetoshelezwa.” ?Umar bin ?Abdil-?Aziyz (Radhiya Allaahu ?anh) amesema maneno yakiwa na maana ifuatayo: 18“Simama pale ambapo walisimama watu, kwa hakika walisimama juu ya elimu na ujuzi. Wao katika kitu kizuri, walikuwa ni wenye nguvu na fadhila kubwa kwa kukifanya hadharani. Ikiwa mtasema: “Kimezuka baada yao, basi hakikuzushwa na yeyote isipokuwa yule anayekwenda kinyume na uongofu wao na kuipa mgongo Sunnah yao. Walionyesha yenye kukidhi na kuzungumza kwa yanayotosheleza. Yaliyo juu ya hayo, ni kujichosha bure na khasara, na yaliyo chini ya hayo ni mapungufu. Kuna watu waliopunguza waliyokuwemo, yakawafanya kuzembea, wakati wengine wakavuka mipaka waliyokuwemo, yakawafanya kupetuka. Baina ya hao 19wawili ndio wako juu ya uongofu uliyonyooka.” Imaam Abu ?Amr al-Awzaa?iy (Radhiya Allaahu ?anh) amesema: “Shikamana na Aathaar za waliotangulia, hata kama watu watakukataa, na 2021jihadhari na maoni ya watu, hata kama watakupambia kwa maneno.” 16 Shaykh Ibn Jibriyn (Rahimahu Allaah) amefafanua neno "Fuata" ifuatavyo: "Fuata Sunnah za Mtume na Maswahabah zake. Fuata njia yao na usizue Bid?ah katika dini." (at-Ta?liyqaat ?alaa matn Lum?at-il-?I?tiqaad, uk. 54, Daar-us-Samiy?iy) 17 ad-Daarimiy (211), at-Twabaraaniy katika ”al-Kabiyr (9/168), al-Laalikaa?iy katika “Sharh Usuul-il- I?tiqaad Ah-is-Sunnah wal-Jamaa?ah” (104), al-Marwaziy katika “as-Sunnah” (23), Ibn Wadhah katika “al-Bid?ah wan-Nahiy anhaa” (10), al-Haythamiy katika “al-Majmah” (1/181). Imaam al-Haythamiy (Rahimahu Allaah) amesema: “Wapokezi wake ni waaminifu.” 18 Shaykh Ibn ?Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) kafafanua neno la Ibn ?Abdil-?Aziyz “watu” namna ifuatayo: “Kinachomaanishwa na wao ni Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) na Maswahabah wake.” (Sharh Lum?at-il-I?tiqaad, uk. 43, Adhwaa?-us-Salaf) 19 Abu Nu?aym (5/338-339) na wengine. 20 Shaykh Ibn ?Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) amefafanua kuhusu "maoni ya watu" yaliyokusudiwa hapa ifuatavyo: "Tahadhari na maoni ya wanachuoni. Hayo ni yale yaliyosemwa kwa kuzingatia maoni peke yake pasi na dalili katika Qur-aan na Sunnah." (Sharh Lum?at-il-I?tiqaad, uk. 44, Adhwaa?-us-Salaf) 17 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy Muhammad bin ?Abdir-Rahmaan al-Adramiy alisema kumwambia mtu ambaye aliongea kwa Bid?ah na akawalingania watu katika Bid?ah hiyo: “Je, hakuijua Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam), Abu Bakr, ?Umar na ?Uthman na ?Aliy au hawakuijua? Yule mtu akasema: “Hapana, hawakuijua.” Akamuuliza: “Kitu ambacho hawakukijua watu hawa umekijua wewe?” Mtu yule akasema: “Basi mimi nasema: "Ndio, walikijua.” Akamuuliza: “Je, yawezekana kweli ikawa hawakukiongelea na wala hawakuwalingania watu juu ya kitu hicho?” Mtu yule akasema: “Ndio, yawezekana.” Akamuuliza tena: “Kitu ambacho hakikuwezekana kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) na makhaliyfah wake ukakiweza wewe?” Mtu yule akaangushwa. Kiongozi akasema na alikuwepo hapo: “Allaah asimrehemu yule ambaye hakuweza yale ambayo 22waliweza wao.” Namna hii ndivyo inavyokuwa kwa yule ambaye hakuweza yale aliyoweza Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam), Maswahabah zake, wale waliowafuata kwa wema, maimamu baada yao na wale wenye msingi madhubuti katika elimu katika kuzisoma Aayah zinazohusu sifa na kusoma maelezo yake na kuzithibitisha kama zilivyokuja – hivyo Allaah asimrehemu mtu huyo. Mfano wa Sifa za Allaah zilizothibitishwa na Qur-aan na Sunnah Miongoni mwa Aayah zilizothibiti kuhusu sifa ni pamoja na maneno ya Allaah (?Azza wa Jall): 21 al-Khatwiyb al-Baghdaadiy katika ”Sharaf Asw-haab-il-Hadiyth” uk. 7, al-Ajjurriy katika “ash- Shari?ah”, uk. 58, Ibn ?Abdil-Barr katika Bayaan Fadhwl-il-?Ilm” (2/114) na wengine. Imaam al- Albaaniy (Rahimahu Allaah) amesema kuwa ni Swahiyh katika “Mukhtaswar-ul-?Uluww”, uk. 138. 22 Tazama Imaam adh-Dhahabiy (Rahimahu Allaah) “Siyar A?laam-in-Nubalaa” (11/314) na Imaam Ibn Kathiyr (Rahimahu Allaah) “al-Bidaayah wan-Nihaayah” (1/335) 18 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy Dalili ya uso wa Allaah ??????,??????? ??????,??? ??, ??????: ?,?,?? ???,?????? ?,??, ????????, ?,?? ,??,”Kila aliyekuwa humo [mbinguni na ardhini] atatoweka. Na utabakia uso wa Mola Wako wenye utukufu na wenye ukarimu." (55:26-27) Dalili ya mikono ya Allaah ?,????,??????? ?,??~?? ???? ”Bali Mikono Yake imefumbuliwa." (05:64) Dalili ya nafsi ya Allaah Allaah (Ta?ala) amesema akielezea kuhusu ?Iysaa (?alayhis-Salaam) ya kwamba atasema: ?????,?, ??, ??? ?????,?? ????? ????,?, ??, ??? ?????,?? ”Unayajua yale yote yaliyomo katika nafsi yangu na wala mimi sijui yale yaliyomo katika Nafsi Yako.” (05:116) Dalili ya kuja kwa Allaah Amesema (Subhaanah): ?,,?, ?,,?, ?????,????? ??,??: ????,??”Na atakapokuja Mola Wako na Malaika safu kwa safu." (89: 22) ?,?,??? ?????????,?? ,?? ?,??? ?,????,,?? ???, ” Je, wanangojea nini isipokuwa Allaah awajie." (02:210) 19 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy Dalili ya kuridhia na kupenda kwa Allaah Amesema (Ta?ala): ?,?,?, ???,?:?? ?????,?, ?,?,??? ???,,: ”Allaah amewawia radhi nao wamemridhia.” (5:119) ?,?,?,??,???? ????,??,?? “Atakaowapenda nao watampenda.” (05:54) Dalili ya kukasirika na kughadhibika kwa Allaah Amesema (Ta?ala) kuhusu makafiri: ?????????, ?,?,??? ???,?,?? ”Na Allaah awaghadhibikie.” (48:06) ?,?,??? ?,?,???? ??? ???,??,?? ????,,?,?? ??????, “Hivyo kwa kuwa wao wamefuata yale yanayomkasirisha Allaah.” (47:28) ?????,??,??,? ?,?,??? ?,???, “Allaah amekirihika kutoka kwao.” (09:46) Dalili ya kuteremka kwa Allaah Katika Sunnah Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) amesema: “Mola Wetu (Tabaarak wa Ta?ala) huteremka kila usiku katika mbingu 23ya dunia.” 23 al-Bukhaariy (1145) na (6321) na Muslim (758). 20 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy Dalili ya kustaajabu kwa Allaah Amesema (Ta?ala): 24“Mola Wako anastaajabu kwa kijana asiyehadaika na mambo ya 25kipuuzi na matamanio.” Dalili ya kucheka kwa Allaah Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) amesema: “Allaah anawacheka watu wawili ambapo mmoja wapo kamuua 26mwingine kisha wote wawili wakaingia Peponi.” Haya na yanayofanana na haya katika yaliyothibiti mlolongo wa wapokezi wake na wapokezi wake wamekubaliwa, tunayaamini na wala hatuyarudishi na wala hatuyakanushi na wala hatuyafasiri kwa maana yenye kwenda kinyume na udhahiri wake. Vilevile hatuyashabihishi na sifa za viumbe na kwa maneno ya wenye kuzua. Tunajua ya kwamba Allaah (Subhaanahu wa Ta?ala) hana yeyote anayeshabihiana na kulingana Naye: ????,????? ?,??,,??? ???,?? ? ?????, ?,???,?,?, ?????? 24 Shaykh Ibn ?Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) amefafanua juu ya "Kustaajabu kwa Allaah" kulikokusudiwa hapa ifuatavyo: "Kuna aina mbili za kustaajabu: Aina ya kwanza: Kustaajabu kwa yule mwenye kustaajabu kufichikana na sababu ya chenye kustaajabisha. Tahamaki anastaajabu na kushangaa pale anapokiona kitu hicho. Aina hii haiwezekani kwa Allaah. Hakuna chochote kinachofichikana kwa Allaah. Aina ya pili: Kustaajabu iwe kunatokamana na kitu kutoka katika mazowea yake au vile kinavyotakiwa kuwa ilihali yule mwenye kustaajabu awe na ujuzi juu ya kitu hicho. Aina hii ndio yenye kuthibiti kwa Allaah (Ta?ala)." (Sharh Lum?at-il-I?tiqaad, uk. 60, Adhwaa?-us-Salaf) 25 Ahmad (4/151), Ibn Abiy ?Aaswim (1/250), Abu Ya?laa (1479), at-Twabaraaniy katika “al-Kabiyr” (17/309), al-Haythamiy (10/270) na wengine. Imaam al-Albaaniy (Rahimahu Allaah) amesema kuwa ni dhaifu katika ”as-Silsilah adh-Dhwa?iyfah” (2426). Lakini Hadiyth iliyopokelewa na Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ?anh) ”Allaah Anastaajabu kwa fulani na fulani... ” ni Swahiyh. (Tazama Swahiyh al-Bukhaariy (4889)). 26 al-Bukhaariy (2826) na Muslim (1890) 21 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy ”Hakuna chochote kinachofanana Naye - Naye ni Mwenye kusikia, Mwenye kuona.” (42:11) Kwa hakika Allaah ni tofauti kabisa na yote yanayomjia mtu akilini na kwenye fikira zake. Dalili ya kwamba Allaah yuko juu ya mbingu na viumbe Katika hayo ni maneno Yake (Ta?ala): ????????? ?????,??? ????, ?,???,?,,??? ”Mwingi wa Rahmah amelingana juu ya ?Arshi." (20:5) ????,,??? ??, ,,? ???,???? ” Je, mnajiaminisha na Yule Aliyeko mbinguni." (67:16) Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) amesema: 27“Mola Wetu ni Allaah Aliye juu ya mbingu, limetakasika jina Lako." Alimwambia (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) mjakazi: “Allaah yuko wapi?” Akasema: “Mbinguni.” Hivyo akasema: “Mwache 28huru, kwani hakika ni muumini." Imepokelewa na Maalik bin Anas, Muslim na maimamu wengine. Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) amesema kumwambia Huswayn: “Unaabudu waungu wangapi?” Akasema: “Saba, sita wako katika ardhi na mmoja Yuko mbinguni.” Mtume akamuuliza: “Ni nani unayemwendea wakati wa matumaini na wakati wa khofu?” Husayn akasema: “Ni Yule ambaye yuko mbinguni.” Mtume akamwambia: “Waache hao sita na mwabudu Yule Aliye mbinguni, na mimi nitakufunza du?aa mbili." Akaingia katika Uislamu na Mtume (Swalla 27 Abu Daawuud (3892), an-Nasaa?iy (1037), al-Haakim (1/344) na (4/218) na wengineo. 28 Muslim (538). 22 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy Allaahu ?alayhi wa sallam) akamfunza aseme: “Eeh Allaah niongoze 29katika uongofu na nikinge na shari ya nafsi yangu." Hali kadhalika katika mambo yaliyopokelewa katika vitabu vya kale, ni kwamba alama za Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) na Maswahabah zake ni kuwa wanasujudu katika ardhi na wanadai kuwa mungu wao yuko mbinguni. Abu Daawuud amepokea katika “as-Sunan” yake ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) amesema: “Kwa hakika umbali wa kati ya mbingu hadi mbingu nyingine ni mwendo wa kadhaa na kadhaa... “ akaendelea kuelezea mpaka alipofikia kusema: “Juu ya hilo kuna ?Arshi na Allaah (Subhaanah) Yuko juu 30yake." Haya na yanayofanana na haya Salaf (Rahimahumu Allaah) wameafikiana kwayo na wameyanukuu na kuyakubali. Hakuna aliyethubutu kuyarudisha, kuyafasiri kimakosa, kuyashabihisha na kuyafananisha. Imaam Maalik bin Anas (Rahimahu Allaah) aliulizwa: 31“Ewe Abu ?Abdillaah! Mwingi wa Rahmah amelingana juu ya ?Arshi. Amelingana namna gani?” Akasema: “Kulingana kunajulikana na namna 29 at-Tirmidhiy (3479), Ahmad (4/444), al-Bukhaariy katika ”at-Taariykh al-Kabiyr” (2/1/1) na wengine. 30 Abu Daawuud (4723), at-Tirmidiy (3320), Ibn Maajah (193), Ahmad (1/206), ad-Daarimiy (1/90-91), Ibn Khuzaymah katika “Kitaab-ut-Tawhiyd” (68) na wengine. 31 Shaykh Swaalih Aalush-Shaykh (Hafidhwahu Allaah) amesema: "Kulingana juu ya ?Arshi ni sifa ambayo Ahl-us-Sunnah wamejipambanua nayo. Watu wa Bid?ah wanapinga kwamba Allaah (Jalla wa ?Alaa) amelingana juu ya ?Arshi Yake. Kuna kundi katika wao ambao wamefasiri "kulingana juu ya ?Arshi" kwamba ni kutawala juu ya ?Arshi. Huku ni kumtukana Allaah (Jalla wa ?Alaa). Allaah (Jalla wa ?Alaa) amesema: ?????,??? ????, ????????? ,??, ???,??? ??,??? ??, ?,?:?,????? ???????,,??? ?????, ??,,?? ?,?,??? ???,,??: ,,?? "Hakika Mola wenu ni Allaah Ambaye Ameumba mbingu na ardhi katika siku sita, kisha akalingana juu ya ?Arshi." (07:54) Amebainisha kuwa kulingana juu ya ?Arshi ni jambo limetokea baada ya kutokuwepo kwake. Hivyo ikifasiriwa kwamba maana yake ni kutawala ni dalili yenye kuonesha kuwa kuna kipindi Allaah (Jalla wa ?Alaa) ambapo alikuwa hafanyi hivo. Huku ni kumtukana Allaah (Jalla wa ?Alaa) kwa sababu ni kumpokonya nguvu na umiliki Wake juu ya viumbe Wake wote. Hili linabainisha na kuthibitisha kwamba kulingana hakuna maana nyingine isiyokuwa ya Ujuu." (Sharh Lum?at-il-I?tiqaad, uk. 73) 23 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy haijulikani. Kuamini hilo ni wajibu na kuulizia hilo ni Bid?ah.” Kisha 32akaamrisha mtu yule atolewe nje." Dalili ya maneno ya Allaah na uwajibu wa kuthibitisha hilo Miongoni mwa sifa za Allaah (Ta?ala) ni kuwa anazungumza kwa maneno ya milele na anamsikilizisha yule anayemtaka katika viumbe Wake. Muusa (?alayhis-Salaam) aliyasikia kutoka Kwake pasi na mkati kati. Vilevile Jibiriy (?alayhis-Salaam) aliyasikia na hali kadhalika Malaika wengine aliyowaidhinisha na Mitume Wake. Hakika Yeye (Subhaanah) atawazungumzisha waumini Aakhirah na [wao waumini] watazungumza Naye. Atawapa idhini wamtembelee. Allaah (Ta?ala) amesema: ??,????,?? ??????? ?,?,??? ??,??,?? ”Na bila shaka Allaah alimzungumzisha Muusa maneno kihakika." (04:164) ???????,???? ????????????? ???,,?? ????, ???????,?,?,? ???,?? ??????? ??? ”Ee Muusa! Hakika Mimi nimekuteua juu ya watu kwa Ujumbe na maneno Yangu." (07:144) ?,?,??? ??,??, ,,? ????,??? ”Miongoni mwao [Mitume kuna] ambaye Allaah alimzungumzisha." (02:253) ????,?, ????:?? ,?? ???? ????,?? ?,??? ?,?,??? ?,?,????,?? ,?? ???,???? ?,??, ????? ”Na wala haikuwa kwa mtu yeyote yule kwamba Allaah amsemeze isipokuwa kwa njia ya Wahy au nyuma ya pazia." (42:51) ??,??: ??,?? ???,?? ??????? ??? ???~??, ??,????? ?,,???, "Basi alipoufikia aliitwa: “Ee Muusa! Hakika Mimi ni Mola Wako." (20:11- 12) ??,?~???,??, ??,?? ?,??? ?,?????? ??? ?,?,??? ??,?? ??,,,?? 32 al-Bayhaqiy katika Kitaab-ul-Asmaa? was-Swifaat” (867) na (868), na ad-Daarimiy katika “ar-Radd ?alaa al-Jahmiyyah” (104), al-Laalakaa?iy (664) na wengine. 24 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy ”Hakika mimi ni Allaah, hakuna mungu wa haki isipokuwa Yeye, basi niabudu." (20:14) Haijuzu kwa mwengine yeyote kusema haya isipokuwa Allaah Pekee. ?Abdullaah bin Mas?uud (Radhiya Allaahu ?anh) amesema: “Allaah anapotamka kwa Wahy, sauti Yake wanaisikia walioko 33mbinguni.” Hilo limepokelewa kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam). ?Abdullaah bin Unays amepokea kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) ya kwamba amesema: “Allaah atawafufua viumbe siku ya Qiyaamah wakiwa uchi, peku, hawakutahiriwa na bila ya kitu na atawanadi kwa sauti watayomsikia walio mbali kama wanavyomsikia walio karibu: “Mimi ndiye mfalme! 34Mimi ndiye Mwenye kuhukumu!"" Imepokelewa na maimamu na al- 35Bukhaariy ameitumia kama dalili. Katika baadhi ya Aathaar imepokelewa ya kwamba Muusa (?alayhis-Salaam) usiku mmoja aliona moto uliyomshtua. Hivyo Mola Wake akamwita: “Ee Muusa!" Akaitika kwa haraka na kwa adabu: “Nakuitikia. Nakuitikia. Naisikia sauti Yako lakini sioni ulipo. Uko wapi?” Akasema: “Mimi niko juu yako, mbele yako, kuliani kwako na kushotoni kwako." Hivyo Muusa akajua kuwa sifa hizi hazimstahikii yeyote isipokuwa Allaah (Ta?ala). Akasema: “Ni Wewe ndiye Mola Wangu. Hivi kweli nasikia maneno Yako Wewe au ni maneno ya 36Mtume Wako?” Akasema: “Hapana, ni maneno Yangu ee Muusa.” 33 Abu Daawuud (4738), Ibn Khuzaymah katika ”Kitaab-ut-Tawhiyd” (95-96), al-Aajurriy katika “ash- Shariy?ah” (294) na wengineo. 34 Imaam al-Albaaniy amesema katika ”Takhriyj-us-Sunnah”: ”Hadiyth Swahiyh.” 35 Tazama al-Bukhaariy (Rahimahu Allaah) katika kitabu ”Adab-ul-Mufrad (970), Khalq Afa?aal-il- ?Ibaad (89) na at-Taariykh al-Kabiyr (7/169). Imekuja pia katika Ahmad (3/490), al-Haakiym (2/437-438), al-Bayhaqiy katika “Kitaab-ul-Asmaa? was-Swifaat” (131) na wengine. 36 as-Suyuutwiy katika ”ad-Durr al-Manthuur” (4/290-292), Ibn-ul-Mundhir, Ibn Abiy Haatim na imenasibishwa pia kwa Ahmad “az-Zuhd”. Tanbihi muhimu! Shaykh Ibn Jibriyn amesema kuhusiana na kisa hapo juu kuhusu Muusa (?alayhis-Salaam): “Kuhusiana na kisa kilichotajwa hapo juu kuhusu Muusa, ni kutoka kwa wana wa Israaiyl ambacho ina maana mtu asikiamini na wala asikirudishe isipokuwa kwa dalili.” (at-Ta?liyqaat ?alaa matn Lum?at-il-?I?tiqaad, uk. 95, Daar-us-Samiy?iy) 25 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy Qur-aan ni maneno ya Allaah hakika Miongoni mwa maneno ya Allaah (Subhaanah) ni Qur-aan tukufu. Nayo ni Kitabu cha Allaah chenye kubainisha, kamba Yake imara na Njia Yake iliyonyooka na ni Uteremsho kutoka kwa Mola wa walimwengu. Umeteremsha Roho Mwaminifu kwenye moyo wa kiongozi wa Mitume kwa lugha ya Kiarabu ulio wazi. Imeteremshwa na wala haikuumbwa, imeanza kutoka Kwake na Kwake ndiko itarudi. Ni Suurah za Muhkamaat, Aayah zilizo wazi, herufi na maneno. Mwenye kuisoma na akaitamka ipasavyo anapata kwa kila herufi moja thawabu kumi. Yana mwanzo na mwisho, sehemu na vipande. Inasomwa kwa midomo, imehifadhi kwenye vifua, inasikizwa kwa masikio na kuandikwa katika misahafu. Ndani yake kuna [Aayah za] Muhkam na za Mutashaabih, zinazofuta na zilizofutwa, ambazo ni maalum na zilizoenea, za maamrisho na za makatazo: ?~??,?, ????,?, ?,??? ?????,?? ?,?,???, ?,?? ????? ?,???~?? ?,???? ,?? ???,?????? ?,????,?? ?,? “Haiingiliwi na batili mbele na nyuma yake - ni Uteremsho kutoka kwa Mwenye hikmah, Mwenye kuhimidiwa." (41:42) Amesema (Ta?ala): ???????, ?,?,???? ?????,?,?? ?,??, ?????? ?,???,?,?? ?,????,?? ??? ?,????,??? ??,???, ???,?,?? ?????,?? ,?? ?????, ,,?,????? ??,????? ???,?,???,? ?,?,,? ??, ”Sema: “Lau watajumuika watu na majini ili walete mfano wa hii Qur-aan, basi hawatoweza kuleta mfano wake japokuwa watakuwa ni wenye kusaidiana."" (17:88) Nacho si kingine ni Kitabu hiki cha Kiarabu ambacho makafiri wamesema juu yake: ?,????,??? ??,?????? ?,????,, ,?? ”Hatutoiamini Qur-aan hii.” (34: 31) Wengine pia wakasema: ???,????? ?????, ?,??? ??,???, ?,?? “Hii si chochote isipokuwa ni maneno ya mtu.” (74:25) 26 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy Hivyo Allaah (Subhaanahu wa Ta?ala) akasema: ???,?? ?,????,?,?? “Nitamumingiza kwenye [Moto wa] Saqar.” (74:26) Vilevile wakasema wengine kwamba ni mashairi. Hivyo Allaah (Ta?ala) akasema: ?,???,? ?,????,?? ???,?, ?,??? ???, ?,?? ? ?,?? ??,??,?? ????? ???,??,?? ?,??,?,,??, ?????”Na hatukumfunza mashairi na wala haistahiki kwake, hii si chochote isipokuwa ni ukumbusho na Qur-aan yenye kubainisha.” (36:69) Baada ya Allaah kuwaraddi ya kwamba ni mashairi na wakati huo huo akathibitisha kuwa ni Qur-aan, hapakubaki utata kwa mtu mwenye busara ya kwamba Qur-aan ni Kitabu hichi cha Kiarabu ambacho kina maneno, herufi na Aayah, kwa sababu kisichokuwa hivyo hawezi yeyote kusema ya kwamba ni mashairi. Amesema (?Azza wa Jall): ?,?,??? ?,??~ ,??? ??,????~???, ???,?~??? ?,???,??? ,??? ???:????? ?????,?, ??,?~???, ?????, ??,??,??, ?,,??? ?????: ??, ????,?, ,???? ”Na ikiwa mko katika shaka kutokana na Tuliyoyateremsha juu ya mja Wetu, basi leteni Suurah moja mfano wake na waiteni mashahidi wenu pasipo na Allaah” (02: 23) Haiwezekani Kwake kuwapa changamoto ya kuleta mfano wa kisichotambulika wala kueleweka. Amesema (Ta?ala): ,?? ?,????~???? ?,?? ??? ?,??,?? ??? ???, ? ?,????~?? ???? ??,???, ?????, ?,????,?? ???,? ??,????,?? ?,??,???? ??? ?,??,,?? ????, ? ????,????? ??,?????? ?????????, ???????? ??,???? ????,?, ????,???? ”Na wanaposomewa Aayah Zetu bayana, wale wasiotarajai kukutana Nasi husema: “Lete Qur-aan isiyokuwa hii au ibadilishe.” Sema: “Hainipasii mimi kuibadilisha kwa khiyari ya nafsi yangu."" (10:15) Kwa hivyo Akathibitisha ya kwamba Qur-aan ni Aayah ambazo wanasomewa. Allaah (Ta?ala) amesema: ?????,??? ??????? ?,??,,?? ?:??~?, ??, ????,????? ?????? ???, ???? ”Bali hizo ni Aayah bayana katika vifua vya wale waliopewa elimu.” (29:49) Amesema (Ta?ala) baada ya kukiapia: ?,???,??,?,??? ?,??? ?,,??,?? ?,? ?,??,?,,? ??????, ??, ??????, ?,????,?? ?,,,?? 27 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy ”Hakika hii bila shaka ni Qur-aan karimu. Katika Kitabu kilichohifadhiwa - hakuna akigusaye isipokuwa waliotakaswa." (56:77-79) Amesema (Ta?ala): ,,??, ”Kaaf Haa Yaa ‘Ayyn Swaad.” (19:01) ??, ?, ”Haa Miym ‘Ayn Siyn Qaaaf.” (42:01-02) Ameanza Suurah ishirini na tisa kwa herufi za kukata. Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) amesema: “Yule ambaye atasoma Qur-aan na akaitamka vizuri, atapata kwa kila herufi moja thawabu kumi, na yule ambaye ataisoma kimakosa, atapata 37kwa kila herufi moja thawabu moja." Hadiyth ni Swahiyh. Amesema (?alayhis-Swalaatu was-Salaam): “Isomeni Qur-aan kabla hawajakuja watu ambao watazisoma herufi zake vizuri pasi na kuvuka koo zao. Wanaharakia kutafuta ujira wake na wala 38hawaiharakii." Abu Bakr na ?Umar (Radhiya Allaahu ?anhumaa) wamesema: “Kuisoma Qur-aan vizuri kunapendekezwa zaidi kwetu kuliko 39kuhifadhi baadhi ya herufi zake." 37 as-Suyuutwiy katika ”al-Haawiy” (1/564) na at-Twabaraaniy katika ”al-Kabiyr” (6021) na pia “al- Awsat”. Tanbihi muhimu! Hadiyth hii ni dhaifu. Imaam al-Haythamiy (Rahimahu Allaah) amesema: “Kumekuja Nahshal na ni mwenye kuachwa.”Nahsal ni Ibn Sa?iyd bin Wardaan al-Wardaaniy na Imaam Ishaaq bin Raahawayh (Rahimahu Allaah) amesema kuwa ni muongo. Tazama “Sharh Lum?at-il-I?tiqaad” uk. 81, ya Ibn ?Uthaymiyn (Rahimahu Allaah), footnote 44, Adhwaa?-us-Salaf. 38 Ahmad (5/338), Abu Daawuud (831) na Ibn Hibbaan (1876). Katika Hadiyth hii kunakuja udhaifu kwa sababu ya Wafaa? bin Shariyh ambaye kaja katika isnadi. Hata hivyo Hadiyth hii imepewa nguvu na Hadiyth zifuatazo, kwa mfano Hadiyth iliyopokelewa na Jaabiyr bin ?Abdillaah (Radhiya Allaahu ?anh) ambayo imekuja pia kwa Ahmad (3/397) na Abu Daawuud (830). Isnadi yake ni Swahiyh ambayo Imaam al-Albaaniy (Rahimahu Allaah) kaitaja katika “as-Silsilah as-Swahiyhah” (259). 39 Ibn Qudaamah katika ”al-Burhaan”, uk. 44, na Ibn Anbaariy katika ”al-Waqf al-Ibtidaa?” (1/20). Tazama “Sharh Lum?at-il-I?tiqaad” uk. 82 ya Shaykh Ibn ?Uthaymiyn (Rahimahu Allaah), footnote 46, Adhwaa?-us-Salaf. 28 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy ?Aliy (Radhiya Allaahu ?anh) amesema: 40“Mwenye kukufuru herufi moja, basi huyo kakufuru Qur-aan nzima." Waislamu wote wamekubaliana juu ya idadi ya Suurah za Qur-aan, Aayah zake, maneno yake na herufi zake. Hakuna tofauti kati ya waislamu ya kwamba mwenye kukanusha kutoka katika Qur-aan, sawa iwe ni Suurah moja, Aayat moja, neno moja au herufi waliyoafikiana kwayo, ya kwamba ni kafiri. Katika hili kuna hoja madhubuti ya kwamba [Qur-aan ni] herufi. Waumini watamuona Mola Wao siku ya Qiyaamah Waumini watamuona Mola Wao Aakhirah kwa macho yao. Watamtembelea, atazungumza nao na wao watazungumza Naye. Allaah (Ta?ala) amesema: ?????,??, ???????: ?????? ?????,?,, ?,?,?????? ?,??,?? ”Kuna nyuso siku hiyo zitanawiri. Zikimtazama Mola wake.” (75:22–23) Amesema (Ta?ala): ?,?????,?,?,,? ?,?,?????? ???????,: ,?, ????,,?? ?,??, “Hapana! Hakika wao siku hiyo watawekewa kizuizi [wasimuone] Mola wao.” (83: 15) Pindi alipowazuia watu hao katika hali ya kuwakasirikia nao, basi ikawa ni dalili ioneshayo ya kwamba waumini watamuona katika hali ya Yeye kuridhika. Vinginevyo kusingelikuwa tofauti baina yao. Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) amesema: “Kwa hakika nyinyi mtamuona Mola Wenu kama mnavyoona mwezi huu 41– hamtosongamana katika kumtazama.” Hadiyth ni Swahiyh iliopokelewa na al-Bukhaariy na Muslim. Ushabihisho huu ni ushabihisho wa maono, na si kwa kitachoonwa, kwa hakika Allaah (Ta?ala) hana anayefanana Naye wala mwenza. 40 Ibn Abiy Shaybah (1/102) na (10/513) na Ibn Jariyr katika ”Jaami?-ul-Bayaam ?an Ta?wiyl Aay-il- Qur-aan” (56) 41 al-Bukhaariy (554) na (574) na Muslim (633). 29 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy Qadhwaa? na Qadar Katika sifa za Allaah (Ta?ala) ni kuwa anafanya kile anachokitaka. Hakiwi kitu isipokuwa kwa kutaka Kwake na wala hakitoki kitu katika utashi Wake. Hakuna kitu ulimwenguni kinachotoka katika makadirio Yake wala katika uendeshaji Wake. Haiwezekani kuepuka Qadar iliyokadiriwa na wala haiwezi mtu hawezi kuvuka yaliyoandikwa katika Ubao uliohifadhiwa. Viumbe wote hutenda kwa matakwa Yake. Lau angeliwalinda wasingemkhalifu. Lau angelitaka wote wamtii wangelimtii. Kaumba viumbe na matendo yao na amekadiria riziki zao na maisha yao. Anamuongoza amtakaye kwa Rahmah Zake na anampoteza amtakaye kwa hekima Yake. Allaah (Ta?ala) amesema: ?,????,???? ???,?? ???,?,?? ?,,?, ???,???? ??? “Haulizwi kwa yale Anayoyafanya, lakini wao wataulizwa." (21:23) ?:?~?,?? ?,??,?,???, ?????, ,??, ?,,?? ”Hakika Sisi tumekiumba kila kitu kwa makadirio." (54:49) ?????~?,?? ?,?:,~?,?, ?????, ,??, ?????,?? ”Na Ameumba kila kitu kisha akakikadiria kipimo sawa sawa.” (25:02) ??,??????,, ,?? ?????, ,??? ??????, ??, ?,??? ???,???,,?? ??, ????? ?,?:?,??? ??, ??????,,? ,?? ????,?? ??? “Hakuna msiba wowote unaokusibuni katika ardhi au katika nafsi zenu isipokuwa umo katika Kitabu kabla Hatujauumba." (57:22) ????????????? ?,?:?~?, ?,???,?? ?,???~???? ,?? ?,?,??? ?~???? ,?,?, ? ??,???, ??,????, ?,?:?~?, ???,?,?? ?,,??,?? ,?? ?~???? ,???? ”Basi yule ambaye Allaah anataka kumhidi humfungulia kifua chake kwa Uislamu. Na yule ambaye anataka kumpoteza humjaalia kifua chake kuwa na dhiki chenye kubana.” (06:125) Ibn ?Umar (Radhiya Allaahu ?anh) amepokea ya kwamba Jibriyl (?alayhis-Salaam) alimuuliza Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam): “Nambie kuhusu imani?” Akasema: “Ni kumuamini Allaah, Malaika Wake, Vitabu Vyake, Mitume Wake, siku ya Mwisho na kheri na shari 30 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy 42ya Qadar." Jibriyl akamwambia: “Umesema kweli." Imepokelewa na Muslim. Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) amesema: 43“Naamini Qadar, kheri na shari yake, mazuri na machungu yake." Miongoni mwa du?aa za Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) ambazo alimfunza al-Hasan bin ?Aliy aombe katika Qunuut ya Witr ni ifuatayo: 44“Nikinge na shari ya Uliyokadiria." Hatufanyi Qadhwaa? na Qadar ni hoja na udhuru kwetu kwa kuacha maamrisho Yake na kujiepusha makatazo Yake. Bali ni wajibu kuamini na kujua ya kwamba ni Allaah ndiye Mwenye hoja juu yetu kwa kuteremsha Vitabu na kuwatuma Mitume. Allaah (Ta?ala) amesema: ????,??? ?~?,?? ??,,?, ?,?,??? ????, ???,,??? ?,??,?? ?,??,?? ”Ili pasikuweko kutoka kwa watu hoja yoyote juu ya Allaah baada ya [kuagizwa] Mitume." (04:165) Tunatambua kuwa Allaah (Subhaanah) hakuamrisha na kukataza isipokuwa ni mambo yanayowezekana kufanya na kuacha. Hali kadhalika hakumtenza nguvu yeyote kufanya maasi au hakumlazimisha kuacha kitu katika utiifu. Allaah (Ta?ala) amesema: ????,???? ?,??? ????,?, ?,?,??? ?,????,?? ??? “Allaah hakalifishi nafsi yoyote ila kwa kadiri ya uwezo wake." (02:286) ?????,?,????? ??? ?,?,??? ???,,???, ”Basi mcheni Allaah muwezavyo." (64:16) ????????? ?????, ??? ???????, ??,?? ???,?, ,??, ?????,?? ????????? 42 al-Bukhaariy (50) na (4777) na Muslim (8). 43 al-Haakim katika ”Ma?rifah ?Uluum-il-Hadiyth” (31) na (32). Tanbihi muhimu! Isnadi dhaifu. Katika isnadi kumekuja Yaziyd ar-Ruqaashiy na ni mdhaifu, na hilo limetajwa katika ”at-Taqriyb” (7683). Imaam an-Nasaa?iy (Rahimahu Allaah) amesema kuhusiana naye: ”Ni mwenye kuachwa.”, na Imaam Ahmad (Rahimahu Allaah) amesema: ”Upokezi unakwenda kinyume na Hadiyth.” na hilo limetajwa katika ”al-Miyzaan” (4/418). 44 Ahmad (1723), Abu Daawuud (1425) na (1426), at-Tirmidhiy (464), an-Nasaa?iy (3/248) na Ibn Maajah (1178). Shaykh Ahmad Shaakir (Rahimahu Allaah) amesema kuwa ni Swahiyh katika taaliki yake ya “Sunan an-Nasaa?iy”. 31 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy ”Leo kila nafsi italipwa kwa yale yote iliyoyachuma, hakuna dhulma leo!" (40:17) Ni dalili yenye kuonesha kuwa mja ana khiyari ya kutenda na kuchuma, analipwa thawabu kwa wema wake na adhabu kwa uovu wake – na haya yanatendeka kwa Qadhwaa? na Qadar ya Allaah. Imani ni maneno na ?amali na inazidi na kupungua Imani ni kutamka kwa ulimi, matendo ya viungo na kuamini moyoni. Inazidi kwa utiifu na inapungua kwa maasi. Allaah (Ta?ala) amesema: ???,????,??? ?,??~ ??????,?? ? ????,,??? ?????????? ?????,,?? ???,??,???? ????,?,?, ?,???~?? ?,?? ?,??,???,?? ?,?,??? ???~???,???? ?,??? ???????? ????? ”Na hawakuamrishwa chochote isipokuwa wamwabudu Allaah wakiwa wenye kumtakasia Yeye dini, kwa imani iliokuwa safi, na wasimamishe swalah na watoe zakaah - na hiyo ndiyo dini iliyosimama imara.” (98:05) Kafanya kumuabudu Allaah (Ta?ala), kuutakasa moyo, kusimamisha swalah na kutoa zakaah, yote hayo yanaingia katika dini. Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) amesema: “Imani ni tanzu sabini na kitu. Ilio juu kabisa ni kusema "nashuhudia ya kwamba hakuna mungu wa haki isipokuwa Allaah... " na ilio chini ni 45kuondoa chenye kudhuru njiani.” Amefanya kutamka na kutenda vyote vinaingia katika katika imani. Amesema (Ta?ala): ??,??,??? ???????~??? ”Huwazidishia imani.” (08:02) ?????,??,??? ?,,? ??,??,??? ???~??~?????? ”Ili awazidishie imani pamoja na imani zao.” (48:04) Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) amesema: 45 al-Bukhaariy (09) na Muslim (35). 32 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy “Atatolewa ndani ya Moto yule aliyesema “hapana mungu wa haki isipokuwa Allaah" na moyoni mwake mna imani kiasi cha punje ya ngano, 46mbegu ya haradali au vumbi nafaka.” Ameifanya imani kuwa inatofautiana. Kuamini ghaibu na yote yaliyosema Mtume Ni ni wajibu kuamini yote aliyoelezea Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) na yamesihi kupokelewa kutoka kwake, sawa tuliyoyashuhudia au yaliyofichikana kwetu. Tunajua ya kwamba ni ya haki na ya kweli, sawa yawe yameingia akilini mwetu au tusiyajue na wala hatukagui uhakika na maana yake. Kwa mfano Hadiyth ya Israa? na Mi?raaj. Hili lilipitika katika hali ya fahamu na haikuwa ndoto. Quraysh wamepinga hilo na hawakupinga ndoto. Mfano mwingine ni Malaika wa mauti alipokuja kwa Muusa (?alayhis-Salaam) ili kuchukua roho yake. Akampiga ngumi na jicho lake likatoka. Akarejea kwa Mola Wake ambapo akamrudishia jicho lake. Mfano mwingine katika hayo ni alama za Qiyaamah, kama kutoka kwa ad-Dajjaal, kuteremka kwa ?Iysaa mwana wa Maryam (?alayhis-Salaam) na kumuua, kutoka kwa Ya?juuj na Ma?juuj, kutoka kwa mnyama, jua kuchomoza kutoka magharibi na yanayofanana na hayo katika [maelezo] yaliyosihi upokeze wake. Adhabu ya kaburi na neema zake ni haki. Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) alikuwa akiomba kinga kutokamana nayo na akaamrisha hilo katika kila swalah. Fitina ya kaburi ni haki, maswali ya Munkar na Nakiyr ni haki na kufufuliwa baada ya kufa ni haki – na hilo ni baada ya Israafiyl (?alayhis- Salaam) kupuliza parapanda: ?,?????,?? ????????: ?????? ????~?,?,??? ?,??? ??, ??,???, ”Basi tahamaki wanatoka makaburini mwao wakienda mbio mbio kwa Mola wao.” (36:51) Watafufuliwa watu siku ya Qiyaamah wakiwa uchi, peku na bila ya kutahiriwa. Watasimama katika kisimamo cha siku ya Qiyaamah mpaka pale ambapo Mtume wetu (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) awashufaie. Allaah (Tabaarak wa Ta?ala) atawafanyia hesabu, itapimwa mizani na vitabu vya ?amali vitagawanywa kwa mkono wa kulia na wa kushoto: 46 al-Bukhaariy (44) na Muslim (193). 33 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy ?,?????, ????:?? ?,??????, ??????? ?,?? ?,????? ??:??????? ?,???,?? ?????? ?????,,???? ???????? ???????, ??????,?? ???????, ?,?,??,???? ?,??????, ??????? ?,?? ?,??,?, ?????,?? ?????,???? ??:????, ??,?~?? ???????, ”Ama yule atakayepewa kitabu chake kuliani mwake, atahesabiwa hesabu nyepesi na atageuka kwa ahli zake akiwa ni mwenye furaha. Na ama yule atakayepewa kitabu chake nyuma ya mgongo wake, ataomba maangamizi na ataingia aungue Moto uwakao.” (84:7-12) Mzani utaopima matendo una vitanga viwili na ulimi: ?,??~????, ??,,???, ??, ???????,,?? ???????, ?,??,,?? ???,??????,?, ?,?,???????? ??,,?, ?,???? ?,??,???,?,??? ???, ???,??????,?, ?,?,???????? ?????,?, ,?,?, ”Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito, hao ndio wenye kufaulu. Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu, basi hao ni wale ambao wamekhasirika nafsi zao, watakuwa katika [Moto wa] Jahannam wenye kudumishwa.” (23:102-103) Mtume wetu Muhammad (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) atakuwa na hodhi siku ya Qiyaamah, maji yake ni meupe kuliko maziwa, matamu kuliko asali na vikombe idadi yake ni sawa na nyote za mbinguni. Mwenye kunywa humo, hatohisi kiu baada yake kamwe. Swiraatw ni haki. Wema watavuka na waasi watatumbukia humo. Mtume wetu (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) ataombea Ummah wake kwa wale walioingia Motoni katika watu wenye madhambi makubwa. Watatolewa kwa uombezi wake baada ya kuunguzwa na kuwa mkaa na majivu, kisha wataingia Peponi kwa uombezi wake. Mitume wengine, waumini na Malaika watakuwa na uombezi pia. Amesema (Ta?ala): ?,??,?,?,?? ?,?????,?, ?,??? ??,?? ???,???:? ?,?,?? ?,??? ?,??,?,?,?? ????? ”Na wala hawamuombei uombezi isipokuwa yule ambaye Amemridhia. Nao kutokana na kumkhofu ni wenye kutahadhari.” (21:28) Kafiri hautomfaa kitu uombezi wa wenye kuombea. 34 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy Pepo, Moto na kifo ni haki Pepo na Moto vimeumbwa na havitotoweka. Pepo ni makazi ya vipenzi Wake na Moto ni adhabu ya maadui Wake. Watu wa Peponi watadumu humo milele: ?,????????? ?,??, ???,?? ?????,?, ??,??,?? ??? ?,??~????, ??,,???, ????,?, ??, ?,??????,?,??? ,,?? ”Hakika wakhalifu wamo kwenye adhabu ya [Moto wa] Jahannam watadumu milele. Hawatopumzishwa nayo nao humo watakata tamaa." (43:74-75) Mauti yataletwa kwa sura ya kondoo mweusi mweupe. Itachinjwa kati ya Pepo na Moto. Kisha kutasemwa: “Enyi watu wa Peponi! Mtadumu na wala hakuna kufa tena! Enyi watu wa Motoni! Mtadumu na wala hakuna kufa 47tena!" Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) ndio wa mwisho na haki zake na Maswahabah wake Muhammad ni Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ?aalyhi wa sallam), ndiye Nabii wa mwisho na ndiye kiongozi wa Mitume. Imani ya mja haisihi mpaka aamini Ujumbe wake na ashuhudie utume wake. Watu hawatofanyiwa hesabu siku ya Qiyaamah isipokuwa baada ya uombezi wake. Hakuna Ummah wowote utaoingia Peponi siku ya Qiyaamah isipokuwa baada ya kuingia kwanza Ummah wake. Yeye ndiye mwenye bendera ya sifa, Cheo kinachosifika na ndiye mwenye hodhi kubwa. Yeye ndiye kiongozi wa Mitume na ndiye muhubiri wao na ndiye mwenye uombezi wao. Ummah wake ndio Ummah bora kabisa na Maswahabah wake ndio wabora kuliko Maswahabah wa Mitume wengine (?alayhimus-Salaam). Mtu bora katika Ummah wake ni Abu Bakr asw-Swiddiyq, kisha ?Umar al-Faaruuq, kisha ?Uthmaan Dhuun-Nuurayn halafu ?Aliy al-Murtadhwaa (Radhiya Allaahu ?anhum). Kutokana na yale yaliyopokea ?Abdullaah bin ?Umar (Radhiya Allaahu ?anhumaa) ambaye amesema: 47 al-Bukhaariy (4730) na Muslim (2849). 35 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy “Tulikuwa tukisema, ilihali Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) bado yuko hai: “Mbora wa Ummah huu baada ya Mitume wake ni Abu Bakr, kisha ?Umar kisha ?Uthmaan kisha ?Aliy." Khabari hizo zinamfikia 48Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) na wala hazikatai."" Kumesihi mapokezi kutoka kwa ?Aliy (Radhiya Allaahu ?anh) ya kwamba amesema: “Mbora wa Ummah huu baada ya Mitume wake ni Abu Bakr, kisha 49?Umar. Lau ningependa, ningemtaja wa tatu." Abud-Dardaa amepokea kutoka kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) ya kwamba amesema: “Jua halijachomoza wala kuzama juu ya yeyote, baada ya Mitume na 50Manabii, kwa aliye bora kuliko Abu Bakr." Yeye ndiye mwenye haki katika viumbe vya Allaah kwa uongozi baada ya Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) kutokana na fadhila zake, kutangulia kwake mbele na Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) kumtanguliza aongoze swalah mbele ya Maswahabah wote (Radhiya Allaahu ?anhum). Maswahabah wote wameafikiana juu ya kumtanguliza mbele na kumpa mkono wa usikivu na utiifu –Allaah asingeacha wote wakaafikiana juu ya upotevu. Baada yake kunakuja ?Umar (Radhiya Allaahu ?anh) kutokana na fadhila zake na Abu Bakr kumpokeza. Kisha anafuata ?Uthmaan (Radhiya Allaahu ?anh) kwa kuteuliwa na waliofanya mashauriano. Kisha anafuata ?Aliy (Radhiya Allaahu ?anh) kutokana na fadhila zake na maafikiano ya waliokuwa wakati wake. Hawa ndio makhaliyfah waongofu ambao Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) amesema juu yao: “Jilazimieni na Sunnah zangu na Sunnah za makhaliyfah wangu waongofu baada yangu. Ziumeni kwa magego." 48 al-Bukhaariy (3655) na (3697). 49 Ahmad (1/106/110) na Ibn Abiy ?Aasim (1201). Imaam al-Albaaniy (Rahimahu Allaah) amesema kuwa ni Swahiyh katika ”Takhriyj-us-Sunnah” (2/570). 50 Ahmad katika ”Fadhaa?il-us-Swahaabah” (135), Abu Nu?aym (3/325), Ibn Abiy ?Aasim (1224) na wengine. 36 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy Vilevile amesema (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam): 51“Uongozi baada yangu utakuwa kwa miaka thelathini." Khaliyfah wa mwisho alikuwa ni ?Aliy (Radhiya Allaahu ?anh). Tunashuhudia watu kumi kuwa Peponi kama walivyowashuhudilia Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) pindi aliposema: “Abu Bakr yuko Peponi, ?Umar yuko Peponi, ?Uthmaan yuko Peponi, ?Aliy yuko Peponi, Twalhah yuko Peponi, az-Zubayr yuko Peponi, Sa?d yuko Peponi, Sa?iyd yuko Peponi, ?Abdur-Rahmaan bin ?Awf yuko 52Peponi na Abu ?Ubaydah bin al-Jarraah yuko Peponi." Kadhalika kila yule ambaye Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) alimshuhudilia Pepo, na sisi pia tunamshuhudilia. Kama aliposema (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam): 53“al-Hasan na al-Husayn ni viongozi wa vijana wa Peponi." Vilevile aliposema kumwambia Thaabit bin Qays: 54“Kwa hakika ni mtu wa Peponi." Hatumkatii muislamu yeyote Pepo wala Moto isipokuwa yule ambaye Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) alimkatia. Lakini hata hivyo tunatarajia mema kwa mwema na tunakhofu kwa mtenda maovu. Hatumkufurishi yeyote katika waislamu kwa sababu ya dhambi na wala hatumtoi katika Uislamu kwa sababu ya ?amali yake. 51 Abu Daawuud (4646), at-Tirmidhiy (2226), Ahmad (5/221), at-Twabaraaniy katika “al-Kabiyr” (6444), al-Hakiym (3/145) na wengine. 52 Abu Daawuud (4649) na (4650), at-Tirmidhiy (3748) na (3757), Ibn Maajah (134), Ahmad (1/187/189) na Ibn Abiy Aasim (1428), (1431) na (1436). Imaam al-Albaaniy (Rahimahu Allaah) amesema kuwa ni Swahiyh katika ”Swahiyh al-Jaami? as-Swaghiyr” (4010). 53 at-Tirmidhiy (3768) na Ahmad (3/166/167). Imaam at-Tirmidhiy (Rahimahu Allaah) amesema ”Hadiyth Hasan na Swahiyh." 54 al-Bukhaariy (3613) na Muslim (119). 37 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy Kupigana Jihaad na viongozi wote, sawa wakiwa ni wema au waovu Tunaonelea kuwa hajj na Jihaad vitaendelea kuwepo na viongozi wote, sawa kiongozi huyo awe ni mwema au muovu. Vilevile inajuzu kuswali swalah ya ijumaa nyuma yao. Anas (Radhiya Allaahu ?anh) amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) amesema: “Mambo matatu ni katika msingi wa imani: Kukomeka na aliyetamka "hakuna mungu wa haki isipokuwa Allaah" hatumkufurishi kwa dhambi hatumtoi katika Uislamu kwa ?amali yake na Jihaad itaendelea kuwepo tangu aliponituma Allaah (?Azza wa Jall) mpaka pale Ummah wangu wa 55mwisho utapopigana na ad-Dajjaal na kuamini Qadar." Imepokelewa na Abu Daawuud. Imani ya Salaf kwa Maswahabah na yule mwenye kuwaponda Miongoni mwa Sunnah ni kuwapenda Maswahabah wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam), kutaja mazuri yao na kuwaombea rahmah, kuwaombea msamaha, kujiweka mbali na kutaja kasoro zao na tofauti iliotokea kati yao, kuamini ubora wao na kutambua kutangulia kwao. Allaah (Ta?ala) amesema: ???,??? ?,??,,???? ?,??, ??,??????, ??, ???,?,?? ????? ?,??,???????? ??,??,???? ?,??,,?? ??,?,????,?????? ??,?? ???,?,? ??,,??: ?,?????,?? ???,?~?,?? ,?? ??????, ?,??,,???? ”Na wale waliokuja baada yao wanasema: “Mola wetu! Tusamehe sisi na ndugu zetu ambao wametutangulia kwa imani na wala usijaalie katika nyoyo zetu mafundo kwa wale walioamini." (59:10) ?????,???? ????,?,?: ?:?,,?,??? ????, ???,~?,?? ?,?,?? ?,??,,???? ? ?,?,??? ?????,: ?~,,?,,? ”Muhammad ni Mtume wa Allaah. Na wale walio pamoja naye ni wakali kwa makafiri wanahurumiana baina yao." (48:29) 55 Abu Daawuud (2532), al-Bayhaqiy (9/159) na wengine. Katika isnadi kuna Yaziyd bin Abiy Nashbah na hajulikani, hilo limetajwa katika ”at-Taqriyb”. Tazama al-Mundhiyr “Mukhtasar Sunan Abiy Daawuud” (3/380). 38 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) amesema: “Msiwatukane Maswahabah wangu. Lau mmoja wenu atatoa dhahabu mfano wa Uhud hawezi kufikia kibaba cha mmoja wao wala nusu 56yake." Imani ya Salaf kwa wakeze Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) Katika Sunnah ni kuwatakia radhi wakeze Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam). Hakika wao ndio wamama wa waumini watwaharifu na wako mbali kabisa na kila chafu. Mbora wao ni Khadiyjah bint Khuwaylid na ?Aaishah 57asw-Swiddiyqah bint asw-Swiddiyq ambaye Allaah amemtakasa katika Kitabu Chake. Ni mke wa Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) duniani na Aakhirah. Atayemshutumu kwa yale Allaah aliyomtakasa, basi atakuwa amemkufuru Allaah mtukutu. 58Mu?aawiyah ni mjomba wa waumini. Alikuwa ni mwandishi wa Wahy wa Allaah na alikuwa ni mmoja wa viongozi wa waislamu (Radhiya Allaahu ?anh). Haki za watawala kwa raia Katika Sunnah ni kuwasikiliza na kuwatii viongozi na watawala wa waislamu na wa waumini. Ni mamoja wawe wema au waovu maadamu hawajaamrisha kumuasi Allaah, katika hali hiyo kutakuwa hakuna utiifu kwa yeyote katika 56 al-Bukhaariy (3673) na Muslim (2541). 57 Mkweli, binti wa mkweli, yaani ni Abu Bakr asw-Swiddiyq (Radhiya Allaahu ?anhumaa). 58 Swahabah mwenye fadhila Mu?aawiyah bin Abiy Sufyaan (Radhiya Allaahu ?anhumaa), kiongozi wa waumini, alikuwa kaka wa Umm Habiybah ambaye ni mmoja wa wake za Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam), kwa hivyo ni mjomba wa waumini. Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah (Rahimahu Allaah) kalijadili suala hili katika ”Minhaj-us-Sunnah” ya kwamba mtu anaweza kuwaita kaka za wake wa Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) wajomba wa waumini au hapana. Tazama ”Minhaj-us-Sunnah” (2/199). 39 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy kumuasi Allaah. Yule ambaye atashika uongozi na wakakubaliana watu kwa hilo na kumridhia – au vilevile ikiwa atashika madaraka kwa nguvu mpaka akawa kiongozi, anakuwa ni kiongozi na huitwa “kiongozi wa waumini" na ni wajibu kumtii na ni haramu kupingana naye, kumfanyia uasi na kuwatawanya waislamu. 59Msimamo wa Ahl-us-Sunnah kwa Ahl-ul-Bid?ah 60Katika Sunnah ni kuwakata Ahl-ul-Bid?ah na kujitenga nao mbali, kuacha 61mijadala na ugomvi katika dini na kutosoma vitabu vya wazushi na 59 Shaykh Swaalih Aalush-Shaykh (Hafidhwahu Allaah) amesema kuhusu kuwaraddi Ahl-ul-Bid?ah ifuatavyo: "Kutilia umuhimu Sunnah na kuwaraddi watu wa Bid?ah ni jambo liko wazi katika hali za maimamu wa Uislamu. Maisha yao yote walikuwa ni wenye kuwaraddi watu wa Bid?ah. Hawakujishughulisha sana na kuwaraddi makafiri katika mayahudi na manaswara. Ukitazama maneno ya Imaam Ahmad, Sufyaan, Hammaad bin Zayd, Hammaad bin Salamah, Nu?aym bin Hammaad, al-Awzaa?iy, Ishaaq, ?Aliy bin al-Madiyniy na wengineo katika maimamu wa Ahl-us-Sunnah utaona kuwa karibu maneno yao yote ilikuwa ni kwa ajili ya kuwaraddi watu wa Bid?ah na kuvunja misingi ya watu wa Bid?ah hata kama watakuwa ni wenye kushikamana na misingi mingine ya Uislamu. Maimamu hawa hawakujishughulisha na kuwaraddi mayahudi na manaswara na imani nyenginezo za kikafiri. Hilo ni kwa sababu shari ya watu wa Bid?ah huwa si yenye kuonekana kwa waislamu na haiaminiki kwa waislamu. Kuhusu shari ya makafiri katika mayahudi na manaswara iko wazi kabisa kwa kila muislamu. Kwa sababu Allaah (Jalla wa ?Alaa) amebainisha hilo katika Qur-aan na hali zao ziko wazi kwa waislamu. Upande mwingine watu wa Bid?ah shari yao ni kubwa zaidi. Si sawa kusema kuwa Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa?ah wamezembea katika kuwaraddi mayahudi na manaswara na badala yake wamejishughulisha na kuwaraddi tu waislamu. Haya yanasemwa na baadhi ya wanafalsafa katika Mu?tazilah na wengineo. Wanasema kuwa Ahl-us-Sunnah wamejishughulisha na kuwaraddi waislamu na kuacha kuwaraddi makafiri katika mayahudi na manaswara na mapote mengine ya kopotevu. Sababu ni ile niliyoibainisha kwamba shari ya Bid?ah ni kubwa zaidi. Hawa wanawajia waislamu kwa kutumia jina la Uislamu. Kuhusu mayahudi na manaswara waislamu tayari ni wenye kuwachukia. Uongofu wa maimamu wa Uislamu ulikuwa wazi juu ya kuwaraddi watu wa Bid?ah na watu wanaofuata matamanio yao. Haikujulikana kuwa walijishughulisha sana na kuwaraddi mayahudi na manaswara. Tukisema hivi haina maana kwamba waumini katika Ahl-us-Sunnah wasijishughulishe na kuwaraddi mayahudi na manaswara. Lakini tunachozungumzia hapa ni ile sifa waliyojitofautisha kwayo maimamu wa Ahl-us-Sunnah. Vinginevyo ni kwamba kumraddi kila ambaye anaushambulia Uislamu, sawa wawe ni makafiri au watu wa Bid?ah, ni jambo la wajibu na faradhi. Lakini isisemwe kwa yule ambaye anawaraddi watu wa Bid?ah ni kwa nini amewaacha mayahudi na manaswara na huwaraddi na kujishughulisha nao. Tunamwambia kuwa huu ndio uongofu wa maimamu wa tangu hapo kale." (Sharh Lum?at-il-I?tiqaad, uk. 156-157) 60 Mtume (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) amesema: 40 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy kutosikiliza maneno yao. Kila jambo jipya katika dini ni Bid?ah na kila mwenye kujiita kwa kitu kingine zaidi ya Uislamu na Sunnah ni mzushi, kama mfano wa Raafidhwah, Jahmiyyah, Khawaarij, Qadariyyah, Murji-ah, Mu?tazilah, Karraamiyyah, Kullaabiyyah na mfano wao - haya ni mapote ya upotevu na vipote vya Bid?ah, Allaah atukinge navyo. Tofauti katika matawi Ama kujinasibisha kwa Imaam fulani katika vitaga vya dini, kama mfano wa madhehebu mane, ni jambo lisilolaumika. Tofauti katika matawi ni rahmah na wanaotofautiana ni wenye kusifiwa kwa kutofautiana kwao. Wanapewa thawabu kwa Ijtihaad zao na tofauti yao ni rahmah kunjufu na kukubaliana kwao [juu ya jambo fulani] ni hoja imara. “Yeyote anayezua au akampokea vizuri mtu wa Bid?ah basi juu yake laana ya Allaah, Malaika wake, na watu wote.” (Imepokewa na al-Bukhaariy (12/41) na Muslim (9/140)) al-Hasan al-Baswriy (Rahimahu Allaah) amesema: “Musishiriki katika vikao vya watu wa Bida'h na watu wenye kufuata matamanio yao, wala musibishane nao, wala musiwasikilize. (Imepokewa katika “Sunan ad-Daarimiy (1/121)) Imaam al-Fudhwayl bin „Iyaad (Rahimahu Allaah) amesema: “Nilikutana na watu walio bora; wote walikuwa ni watu walioshikamana na Sunnah na wote walikuwa wakikataza kuandamana na watu wa Bida'h.” (Hilyat-ul-Awliyaa? (8/103) ya Imaam Abu Nu?aym (Rahimahu Allaa).). 61 Imaam Ibn Khuzaymah (Rahimahu Allaah) amesema alipoulizwa kuhusiana baadhi ya vitabu vya Ahl-ul-Bid?ah kuhusu Majina na Sifa za Allaah: “Ni Bid?ah waliyozua! Maimamu wa Waislamu, wanaume wa madhehebu na maimamu wa Waislamu kama mfano wa Maalik, Sufyaan, al-Awzaa?iy, ash-Shaaf?iy, Ahmad, Ishaaq, Yahyaa bin Yahyaa, Ibn-ul-Mubaarak, Muhammad bin Yahyaa, Abu Haniyfah, Muhammad bin al-Hasan na Abu Yusuf waliwapuuza. Walikuwa wakivitahadharisha na kukataza kuviingilia. Badala yake walikuwa wakiwaelekeza wafuasi wao katika Kitabu na Sunnah. Hivyo ndio maana nakutahadharisha kuangalia vitabu vyao!” (al-Istiqaamah (1/108) cha Imaam Ibn Taymiyyah (Rahimahu Allaah).) 41 www.wanachuoni.com Lum?at-ul-I?tiqaad Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy Hitimisho Tunamuomba Allaah atukinge na Bid?ah na fitina, atufufue na Uislamu na Sunnah, atujaalie ni miongoni mwa wenye kumfuata Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ?alayhi wa sallam) katika maisha haya na atukusanye na watu wake baada ya kufa kwetu kwa fahmah na fadhila Zake. Aamiyn. Hapa ndio mwisho wa kitabu. Himdi zote ni Zake Allaah Mmoja, na swalah na salaam zimwendee kiongozi wetu Muhammad, kizazi chake na Maswahabah zake wote. 42 www.wanachuoni.com
本文档为【Lum 180;at-ul-I 180;tiqaad – Imaam Ibn Qudaamah al-Maqdisiy】,请使用软件OFFICE或WPS软件打开。作品中的文字与图均可以修改和编辑, 图片更改请在作品中右键图片并更换,文字修改请直接点击文字进行修改,也可以新增和删除文档中的内容。
该文档来自用户分享,如有侵权行为请发邮件ishare@vip.sina.com联系网站客服,我们会及时删除。
[版权声明] 本站所有资料为用户分享产生,若发现您的权利被侵害,请联系客服邮件isharekefu@iask.cn,我们尽快处理。
本作品所展示的图片、画像、字体、音乐的版权可能需版权方额外授权,请谨慎使用。
网站提供的党政主题相关内容(国旗、国徽、党徽..)目的在于配合国家政策宣传,仅限个人学习分享使用,禁止用于任何广告和商用目的。
下载需要: 免费 已有0 人下载
最新资料
资料动态
专题动态
is_601191
暂无简介~
格式:doc
大小:228KB
软件:Word
页数:0
分类:
上传时间:2017-12-06
浏览量:69